Ebenezer Revival International Ministry Ebenezer Revival International Ministry
-
- Religion & Spirituality
Karibu katika Kanisa la Ebenezer Revival International Ministry na Nabii Analyce Ichwekeleza.
-
Juni ni Mwezi Wa Habari Njema - Nabii Analyce Ichwekeleza
Mwezi wa sita malaika Gabriel alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, kumpa habari njema Mariamu. Jiunge nasi katika neno hili na ujifunze jinsi Mungu anavyoleta habari njema katika maisha yetu kupitia vyanzo mbalimbali.
-
Kupokea Sehemu ya Roho Aliyonayo Mtumishi wa Mungu - Nabii Analyse Ichwekeleza
.2 Wafalme 2 : 1 - 18
Elia akamwambia Elisha, “Niambie unalotaka nikufanyie kabla sijaondolewa kwako.”
Elisha akamwambia, “Naomba sehemu maradufu ya roho yako.”
Elia akajibu, “Ombi lako ni gumu, hata hivyo utakipokea kipawa changu hicho ikiwa utaniona wakati nitakapoondolewa kwako; lakini usiponiona, basi hutapewa.” -
Kukua Kiroho (Part 2) - Nabii Analyce Ichwekeleza
Kwa maana sisi ni matokeo ya kazi ya Mungu tulioumbwa katika Kristo Yesu, ili tuwe na matendo mema ambayo Mungu alikwisha andaa, tuishi katika hayo. (Waefeso 2:10)
-
Kukua Kiroho - Nabii Analyce Ichwekeleza
Kama vile watoto wachanga wanavyotamani maziwa, nanyi pia mnapaswa kuwa na hamu ya maziwa halisi ya kiroho, ili kwa nguvu yake mpate kukua na kukombolewa.
(1 Petro 2:2) -
Kuteka Baraka Za Wazazi (PART 2) - Nabii Analyce Ichwekeleza
Ukweli ni kwamba, wazazi ni watu wa muhimu sana kwako bila kujali hali zao za kiroho. Wana upekee fulani katika maisha yako. Kwa maana kupitia wao,wewe ulizaliwa. Upekee huu ni kuhusu “baraka” ambazo Mungu ameruhusu kuziweka kwa wazazi wako.
-
Kuteka Baraka Za Wazazi - Nabii Analyce Ichwekeleza
Waheshimu baba na mama yako upate baraka ( Waefeso 6:2-3). Kuna mambo mengine unayopitia ni kwa sababu mioyo ya wazazi wako ( wa kiroho au wa kimwili) imefunga! Ujue kufanikiwa kwako kutakuwa ni kugumu sana. Maana kuna watu ambao waliondoka nyumbani kwa wazazi au walezi wao kwa mafarakano kisha hawajarudi mpaka wazazi wamekufa,au hawajarudi mpaka leo.