Wanawake wa Imani Soma Biblia
-
- 宗教/スピリチュアル
Vipindi vya wanawake wa Kikristo. Masungumso kuhusu mambo ya maisha. Vipindi vyote ni Kiswahili.
-
Kupendwa na Mungu
Je, umezingatia kwamba sisi wanawake tunacho kitu kama sanduku mioyoni mwetu. Sehemu inayopaswa kujaa upendo. Ni jinsi Mungu alivyotuumba. Lakini mara nyingi ninasikia utupu hapo, au tuseme nina kiu. Kiu ya kupendwa. Ebu fikiria ungeambiwa maneno matamu haya: “mna thamani mbele yangu, kwa kuwa nimewapa hadhi na kuwapenda.” Haya ni maneno ya Mungu.
-
Anakupenda kwa sababu Alikuumba
Tunafahamu kwamba tuna shida mbalimbali katika maisha yetu. Shida ya uchumi ni rahisi kutambua, na wengi wanapambana kila siku ili wapate hata kidogo tu cha kulisha familia. Kwa nini Mungu haoni hali hii na kunisaidia kama ananipenda?
-
Yesu anapiga Hodi Kwako
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.
Uf. 3:20 -
Mwanamke Msamaria anawekwa huru na Yesu
Mwanamke tutakayemkuta leo alikuwa anatafuta upendo, uhuru na amani kama tulivyoongea kipindi kingine, sisi wote tunatafuta mambo haya juu ya mambo yote mengine. Lakini huyu mwanamke pale alipoangalia na kutafuta, hakuweza kuyapata. Labda pia wewe uko kwenye hali ya kutafuta sana upendo, uhuru na amani, lakini baado hujayapata vizuri. Labda unaangalia mahali ambapo haipo!
-
Ushuhuda wa Dorena Jakobo 1
Mama Neema anaongea na Dorena Jakobo aliyekutana na vikwazo vingi maishani mwake.
-
Ushuhuda wa Dorena Jakobo 2/2
Mama Neema anaongea na Dorena Jakobo, "Mama Eliyah", kuhusu jinsi baba yake Dorena, aliokoka kupitia yeye.