66 avsnitt

Nukta Habari inakusogeza na mambo mtambuka yanayokuhusu ikiwemo burudani, mtindo maisha, safari, teknolojia na biashara.

Nukta the Podcast Nukta Habari

    • Nyheter

Nukta Habari inakusogeza na mambo mtambuka yanayokuhusu ikiwemo burudani, mtindo maisha, safari, teknolojia na biashara.

    Restoration of Lake Manyara Tilapia remains an uphill duty

    Restoration of Lake Manyara Tilapia remains an uphill duty

    Join Daniel Samson to explore in detail about endangered Manyara Tilapia in Lake Manyara.

    Stocks of Manyara tilapias have plummeted to alarmingly low levels in recent decades due to unsustainable fishing. 

    The International Union for Conservation of Nature (IUCN) Red List of Threatened Species Report 2006 shows that the area of occurrence of the fish, which previously accounted for 73.6% of the total catch in the region, has shrunk from 5,000 km2 to 1800 km2 in recent decades.

    As a result, the fish is now listed as an endangered species by the IUCN because of driving forces, including overfishing and pollution.

    The fish can only be found in the soda lakes of north-central Tanzania: Lakes Manyara, Kitangiri, Singida, Kindai, and Sulunga. 

    Researchers argue that 20 years have passed since the last estimation of fish caught from Lake Manyara. The current stock of Tilapia in the lake is unknown.

    The lake's proximity to villages, including Barabarani, Migombani, Majengo, and Oltukai, has led to an overdependence on its resources, with many locals relying on fishing for daily sustenance. 

    Using illegal nets to maximize catches has further exacerbated the problem, significantly reducing fish populations and shifting towards smaller-sized fish.

    • 10 min
    From sunlight to harvest: How solar energy brings hopes to farmers in Iringa

    From sunlight to harvest: How solar energy brings hopes to farmers in Iringa

    For decades, farmers in Lupembe Lwa Senga village in Iringa region had relied on the traditional farming system for their livelihoods. Apart from using hand hoes, animal plows, they would wait for the rain to irrigate their crops.  

    For small plots like gardens, they would use buckets or recently fuel-powered water pumps for irrigation. 

    “We started irrigation farming as a group in1999, by that time we were using a fuel-powered pump with the cost of 200,000 for buying petrol to irrigate all five acres a day, it was terrible,” Gabriel Mmewa, farmer in Lupembe Lwa Senga said. .

    With outdated oil pump machines driving the irrigation process, he said the cost of production soared, leaving the farmers trapped in a cycle of diminishing returns.

    However, as the demands of a growing population and the uncertainties of rains, the need for innovation became apparent.

    • 7 min
    UPUNGUFU WA WALIMU SHULE YA MSINGI UNAVYOATHIRI ELIMU TANZANIA

    UPUNGUFU WA WALIMU SHULE YA MSINGI UNAVYOATHIRI ELIMU TANZANIA

    Wakati watahiniwa zaidi ya milioni moja wa elimu ya msingi Tanzania Bara wakiwa wanasubiri hatma yao, baada ya kumaliza mitihani yao jana Septemba 14, 2023, utoshelevu wa walimu katika ngazi hiyo muhimu ya elimu kwa shule za Serikali umeendelea kuwa kitendawili

    Kitabu cha hali ya uchumi cha mwaka 2022, kinabainisha kuwa mpaka Disemba mwaka 2022 kulikuwa na jumla ya wanafunzi milioni 10.8 katika shule za msingi za Serikali Tanzania, huku idadi ya walimu katika shule za Serikali ikiwa 173,276.

    Hii ni sawa na kusema idadi ya wanafunzi waliopo ni mara 62 zaidi ya idadi ya walimu na hivyo kwa wastani mwalimu mmoja hufundisha darasa lenye wanafunzi 63 kwa wakati mmoja uwiano ambao uko juu ya kiwango kinachotakiwa cha wanafunzi 45 kwa darasa.

    Aidha, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) inataja Wilaya ya Kasulu, mkoani Kigoma kuwa ndio wilaya ambayo mwalimu mmoja hufundisha darasa lenye wanafunzi wengi zaidi wanaofika 103.

    Wilaya ya Muleba iliyopo mkoani Kagera ndiyo wilaya pekee iliyofanikiwa kufikia uwiano stahiki kwa wanafunzi 45 kufundishwa na mwalimu mmoja kwa darasa mwaka 2021.


    Wadau wa elimu nchini Tanzania, wanatoa maoni yao juu ya namna upungufu wa walimu shule za msingi unavyoathiri sekta ya elimu nchini.

    Karibu.

    • 9 min
    Elimu ya Veta inavyowainua walemavu wa akili Tanzania

    Elimu ya Veta inavyowainua walemavu wa akili Tanzania

    Awali, ilikuwa ni vigumu kushuhudia watu wanaozaliwa na ulemavu wakipata huduma muhimu wanazozihitaji kama elimu, afya, pamoja na kushirikiana na wanajamii wengine kuibua suluhu za matatizo yanayozikabili jamii zao.

    Hivi sasa zama hizo zimepita. Kutokana na hatua zilizochukuliwa na Serikali pamoja na wadau, ikiwemo kuielimisha jamii kutowabagua na kushirikiana na kundi hilo, kama binadamu wengine watu wenye ulemavu nao wanapata huduma wanazostahili.

    Miongoni mwao ni kijana Paulo Ngunyali, mhitimu wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) kilichopo Chang’ombe, Jijini Dar es Salaam. Pamoja kuwa mlemavu wa akili amehitimu fani ya uundaji wa mashine, na sasa ni mwalimu msaidizi katika kitengo cha watu wenye mahitaji maalumu.

    Katika maonesho ya kimataifa ya kibiashara maarufu kama Saba Saba, Paulo (32), amekuwa kivutio cha wengi kutokana na namna anavyoelezea kwa ufasaha jinsi mashine ya kupima uwezo wa kufundishaa  watu wenye ulemavu wa akili inavyofanya kazi.

    • 8 min
    MFAHAMU MBUNIFU WA MAJIKO YANAYOTUMIA MAWE TANZANIA

    MFAHAMU MBUNIFU WA MAJIKO YANAYOTUMIA MAWE TANZANIA

    Nishati ya kupikia ni miongoni mwa mahitaji muhimu ya binadamu duniani kote, hiyo ndio huwezesha mapishi ya aina mbalimbali za vyakula tunavyokula ili kuimarisha afya na kuwezesha utendaji wa shughuli za kila siku.

    Watu wengi wanatambua gesi, mkaa, umeme, mafuta pamoja na kuni kama ndio vyanzo vya nishati ya kupikia kwa kuwa ndio ambavyo vinatumika kwa kiasi kikubwa kwa sasa huku jitihada nyingi zikielekezwa kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia.

    Hata hivyo, jijini Dar es Salaam kuna ubunifu mpya wa nishati ya kupikia inayotumia mawe, ambapo inatajwa kupunguza kwa kiasi kikubwa gharama za kupikia kwa gesi, umeme, mkaa au nishati nyingine.

    Ndiyo! Ubunifu, udadisi pamoja na uthubutu umewezesha ugunduzi huu ambapo sasa mawe yanayopatikana kwa urahisi katika maeneo mengi nchini Tanzania yanaweza kutumika kama chanzo cha nishati ya kupikia.

    Raymond James (25) maarufu kama Mr Majiko, ndiye mbunifu wa majiko hayo yanayotumia mawe, umeme kidogo pamoja na chenga za mkaa mbadala zinazotokana na vifuu vya nazi.

    Kijana huyo mkazi wa Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam, ameiambia Nukta Habari kuwa kukosa ajira ndio sababu kubwa iliyommchochea kubuni majiko hayo ili aweze kujiingizia kipato kitakachomuwezesha kuendesha maisha.

    Katika podcast hii, amezungumza mengi. karibu kumsikiliza

    • 7 min
    JINSI MATAPELI WANAVYOTUMIA TAASISI YA MO FOUNDATION KUIBIA WATU

    JINSI MATAPELI WANAVYOTUMIA TAASISI YA MO FOUNDATION KUIBIA WATU

     Kama wewe ni mtumiaji wa mtandao wa Facebook huenda umewahi kukutana na chapisho linalohusu fursa ya mikopo kutoka kwenye taasisi ya mfanyabiashara bilionea nchini Tanzania Mohamed Dewji Foundation

    Sehemu ya chapisho hilo lianasomeka ‘𝐉𝐈𝐏𝐀𝐓𝐈𝐄 𝐌𝐊𝐎𝐏𝐎 𝐊𝐔𝐓𝐎𝐊𝐀 𝐌𝐎𝐇𝐀𝐌𝐄𝐃 𝐃𝐄𝐖𝐉𝐈 𝐅𝐎𝐔𝐍𝐃𝐀𝐓𝐈𝐎𝐍 kwa maelekezo ya kupata vigezo na masharti njoo hwatspp kwa no👉🏿 0748923136’.

    Chapisho hilo pamoja na kuhamasisha watu kuomba mikopo wametaja kigezo cha kutoa kwanza kiasi cha hisa ya mkopo unaotaka kupewa kabla ya kupata mkopo wenyewe.

    Ufafanuzi zaidi wa taarifa hiyo unaonesha kama unahitaji kukopa Sh100,000 basi utalazimika kutoa kwanza hisa ya Sh22,000 ndipo upewe mkopo huo.

    Taarifa hiyo imesambaa katika mtandao wa Facebook kupitia akaunti zenye majina tofauti tofauti toka mwaka 2022  huku ikiwa imeambatanishwa na  video fupi inayomnukuu Mohamed Dewji kuwa anatoa mikopo.

    Hata hivyo, Habari hiyo haina ukweli wowote kwa kuwa ni habari za uzushi zinazotumiwa na matapeli kuwalaghai wananchi na kujipatia vipato kwa njia zisizo halali. 




    Nukta Fakti imefanya utafiti ili kubaini ukweli wa akaunti hizo za mtandao wa Facebook na kugundua kuwa akaunti hizo hazina uhusiano wowote na Mohamed Dewji mwenyewe au taasisi yake ya Mohamed Dewji Foundation.

    Akaunti sahihi ya Facebook ya mfanyabiashara huyo maarufu nchini ni Mohammed Dewji huku ile ya taasisi yake ni Mo Dewji Foundation na sio Mikopo Tanzania kama inavyojitambulisha akaunti hiyo inayodai kutoa mikopo.

    Mohamed Dewji hatoi mikopo

    Utafiti zaidi uliofanywa na Nukta Fakti umebaini kuwa, si Mohamed Dewji mwenyewe wala taasisi yake ambayo inajihusisha na utoaji wa mikopo kwa namna yoyote ile.

    Kupitia mtandao wa Linkedin Mohamed Dewji amewahi kutoa taarifa kwa umma akifafanua kuwa taasisi yake inajihusisha zaidi kutoa misaada ya kielimu kwa kufadhili masomo, upatikanaji wa maji pamoja na kutatua changamoto katika sekta ya afya.

    • 7 min

Mest populära poddar inom Nyheter

Fupar & fall
Third Ear Studio
Det politiska spelet
Sveriges Radio
USApodden
Sveriges Radio
Eftermiddag i P3
Sveriges Radio
Radiokorrespondenterna Ryssland
Sveriges Radio
Dagens Eko
Sveriges Radio