![](/assets/artwork/1x1-42817eea7ade52607a760cbee00d1495.gif)
24 episodios
![](/assets/artwork/1x1-42817eea7ade52607a760cbee00d1495.gif)
Jukwaa la Michezo RFI Kiswahili
-
- Deportes
Makala haya yanaangazia maendeleo ya michezo mbalimbali Ulimwenguni na pia huwa haiwaweki kando wanamichezo waliobobea na vilevile kufanya uchanganuzi wa kina wa michezo wakati wa mashindano mbalimbali.
-
Kipyegon, Omanyala wafuzu Olimpiki ya Paris kwenye mchujo wa kitaifa
Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na mchujo wa kitaifa wa Kenya kuteua timu itakayowakilisha kwenye Olimpiki ya Paris mwaka huu, Kenya yakosa kupandishwa daraja kwenye tenisi mashindano ya Billie Jean King Cup, uwanja wa Amahoro nchini Rwanda umeidhinishwa na FIFA kuandaa mechi za kimataifa, Junior Starlets ipo guu moja kufuzu Kombe la Dunia, droo ya kufuzu AFCON 2025 kuandaliwa Julai na michuano ya EURO kuanza Ujerumani.
-
French Open: Iga Swiatek ashinda ubingwa wake wa nne wa Roland Garros
Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na uchambuzi wa mechi za kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2026 (Afrika), Kenya kuandaa mashindano ya mchujo kutafuta timu itakayowakilisha katika Olimpîki ya Paris mwezi Julai huku wanamichezo 33 wakipigwa na marufuku kwa kutumia dawa za kusisimua misuli, matokeo ya Congo Cup, kocha Gamondi arefusha mkataba wake klabuni Yanga huku zikiwa zimesalia siku sita kabla ya mashindano ya EURO nchini Ujerumani, Iga Swiatek ashinda ubingwa wake wa nne wa French Open
-
BAL2024: Petro de Luanda yaibuka na taji la Ligi ya Basketboli barani Afrika
Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa fainali ya Ligi ya Basketboli Afrika mwaka huu, matokeo ya Diamond League mkondo wa Oslo na mchujo wa raga duniani, uchambuzi wa vikosi vya Afrika Mashariki na Kati kuelekea mechi za kufuzu Kombe la Dunia la mwaka 2026, uchambuzi wa Fainali ya Klabu bingwa Ulaya (Dortmund dhidi ya Real Madrid) na matokeo ya French Open huku Ronaldo akitokwa na machozi baada ya kupoteza fainali ya Saudi Kings Cup
-
DRC: Sebastian Desabre arefusha mkataba wake kama kocha wa timu ya taifa
Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa fainali ya Klabu bingwa Afrika, Tanzania waibuka na kombe la shule za upili afrika mchezo wa soka, fainali za ligi ya basketboli kuanza nchini Rwanda wakati makocha wa Kenya na Uganda wataja vikosi vyao kufuzu Kombe la Dunia na matokeo ya Ligi za ulaya.
-
CAF: Nani ataibuka na taji la Klabu bingwa barani Afrika 2024?
Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa fainali ya Klabu Bingwa Afrika mwaka 2024, Zanzibar kuandaa fainali za mashindano ya shule za upili barani Afrika, Mkusanyiko wa michezo kwenye ukanda wa Afrika Mashariki, Maniema yarejea kwenye mashindano ya vilabu barani Afrika, uchambuzi wa mbio za kuwania taji la Uingereza kati ya Man City na Arsenal, Ngolo Kante arejea kikosini mwa Ufaransa, Brazil yateuliwa kuandaa Kombe la Dunia la kina dada la mwaka 2027.
-
Diamond League: Mary Moraa na Beatrice Chebet waibuka washindi riadha za Doha DL
Tuliyokuandalia hii leo ni pamoja na matokeo ya riadha kwenye Doha Diamond League, AFCON UAE kuanza hapo kesho huko Dubai, michuano ya Congo Cup, uchambuzi wa mechi za Ligi ya Basketboli ya Afrika, Guinea yafuzu fainali za Olimpiki kwenye soka, mechi za kufuzu Kombe la Dunia la U17 kwa kina dada, Mbappe atangaza rasmi kuondoka PSG na uchambuzi wa fainali za mwaka huu za michuano ya bara Ulaya.