1 hr 7 min

Ep. 30 - Salama Na SEVEN | ROCKSTAR Salama Na

    • Entertainment News

Mtaani huwa wanasema ‘hizo kazi za wanaume’, maana mambo ya kukesha na watoto wa kiume na kuhangaika nao usiku na mchana kwa mwanamke inakua ngumu, na pengine inaweza ikaleta mambo yasiyohusu au ikasababisha vitu nyengine visiende kwasababu tu anayefanya hiyo kazi ni MWANAMKE. Ila kwa Christine ‘Seven’ Mosha nadhani hayo maneno yalikua ndo mafuta kwenye utambi wake na aliyatumia hayo kuweza kutoa mwanga maridhawa ulioset standard ya kuvutia. Kuna kipindi na mpaka sasa, ukiwataja ma meneja wa wasanii walio hodari hapa kwetu basi la Seven litakua la kwanza kwa mujibu wangu Mimi, maana kwa kuwa mfano kwenye tasnia aliweza haswa!

So swali ni alifikaje huko? Kabla hatujafika huko niseme ambavyo mimi namfahamu yeye rafiki yangu huyu. Kwanza hatupishani umri kabisa na pili nimekua fan wake wa muda mrefu. Napenda jinsi anavyojibeba. Napenda anavyojiweka, anavyofanya mambo yake, anavyokua bora kila miaka inavyozidi kwenda lakini kikubwa zaidi ni jinsi anavyojua mziki wetu na anavyopambana kuweka kipaji chake na cha wale anaowasisamia vizuri sana, na haswa ukimuacha akuongoze kwa mfano. Nayasema haya kwasababu nna idea ya jinsi anavyowaona watu na vipaji vyao na anavyotaka kuwanyooshea yao kwa moyo mmoja ili yao na yake yaende vizuri sana. Kwenye tasnia ambayo imejaa wanaume yeye ameweza kukaa miaka yote hiyo na huku akihakikisha heshima na maendeleo yake na anayewaongoza yakiongea yenyewe.

Kwenye kikao hiki nilitaka kumfahamu kwa undani haswa kwa faida yetu sote lakini kama kawaida, alikua mgumu kuongelea maisha yake binafsi, na unaweza kumuelewa maana si kila mtu anapenda kuyaanika maisha yake na ya awapemdao hadharani, so tuligusia tu kwa uchache lakini tuliongelea sana mambo ya biashara, muziki, Ali, Lady JD, Ommy Dimpoz, Rockstar yake na jinsi alivyoanza na mpaka hapa alipo. Pia tuliongelea mahusiano yake na Marehemu Ruge Mutahaba na enzi hizo alivyoanza kama mtangazaji wa radio na kufikia level ya kusimamia talanta za watu wengine. Seven alianza na TID wakati huo hata usimamizi wa vipaji halikua jambo muhimu.

Pia Seven si mtu wa kutopenda kuwa mbele mbele kama mfuko wa shati, na kwa uelewa wangu anapenda mnoo kuona watu wanakua na wanafaidika na vipaji vyao walivyopewa na Mwenyezi Mungu. Je game imekua kiasi gani? Muelekeo wetu je, tunaelekea kuzuri? Tunakua? Nini tufanye ili watu wafaidike zaidi? Kuna hayo na mwengine ya kumwaga katika maongezi yetu haya, na yangu matumaini utamfahamu zaidi Christine na kumpa heshima yake anayostahili. Tafadhali enjoy.

Love,

Salama.



Follow:

Twitter: http://twitter.com/YahStoneTown

Instagram: http://Instagram.com/YahStoneTown

Facebook: http://facebook.com/YahStoneTown


---

Support this podcast: https://podcasters.spotify.com/pod/show/yahstonetown/support

Mtaani huwa wanasema ‘hizo kazi za wanaume’, maana mambo ya kukesha na watoto wa kiume na kuhangaika nao usiku na mchana kwa mwanamke inakua ngumu, na pengine inaweza ikaleta mambo yasiyohusu au ikasababisha vitu nyengine visiende kwasababu tu anayefanya hiyo kazi ni MWANAMKE. Ila kwa Christine ‘Seven’ Mosha nadhani hayo maneno yalikua ndo mafuta kwenye utambi wake na aliyatumia hayo kuweza kutoa mwanga maridhawa ulioset standard ya kuvutia. Kuna kipindi na mpaka sasa, ukiwataja ma meneja wa wasanii walio hodari hapa kwetu basi la Seven litakua la kwanza kwa mujibu wangu Mimi, maana kwa kuwa mfano kwenye tasnia aliweza haswa!

So swali ni alifikaje huko? Kabla hatujafika huko niseme ambavyo mimi namfahamu yeye rafiki yangu huyu. Kwanza hatupishani umri kabisa na pili nimekua fan wake wa muda mrefu. Napenda jinsi anavyojibeba. Napenda anavyojiweka, anavyofanya mambo yake, anavyokua bora kila miaka inavyozidi kwenda lakini kikubwa zaidi ni jinsi anavyojua mziki wetu na anavyopambana kuweka kipaji chake na cha wale anaowasisamia vizuri sana, na haswa ukimuacha akuongoze kwa mfano. Nayasema haya kwasababu nna idea ya jinsi anavyowaona watu na vipaji vyao na anavyotaka kuwanyooshea yao kwa moyo mmoja ili yao na yake yaende vizuri sana. Kwenye tasnia ambayo imejaa wanaume yeye ameweza kukaa miaka yote hiyo na huku akihakikisha heshima na maendeleo yake na anayewaongoza yakiongea yenyewe.

Kwenye kikao hiki nilitaka kumfahamu kwa undani haswa kwa faida yetu sote lakini kama kawaida, alikua mgumu kuongelea maisha yake binafsi, na unaweza kumuelewa maana si kila mtu anapenda kuyaanika maisha yake na ya awapemdao hadharani, so tuligusia tu kwa uchache lakini tuliongelea sana mambo ya biashara, muziki, Ali, Lady JD, Ommy Dimpoz, Rockstar yake na jinsi alivyoanza na mpaka hapa alipo. Pia tuliongelea mahusiano yake na Marehemu Ruge Mutahaba na enzi hizo alivyoanza kama mtangazaji wa radio na kufikia level ya kusimamia talanta za watu wengine. Seven alianza na TID wakati huo hata usimamizi wa vipaji halikua jambo muhimu.

Pia Seven si mtu wa kutopenda kuwa mbele mbele kama mfuko wa shati, na kwa uelewa wangu anapenda mnoo kuona watu wanakua na wanafaidika na vipaji vyao walivyopewa na Mwenyezi Mungu. Je game imekua kiasi gani? Muelekeo wetu je, tunaelekea kuzuri? Tunakua? Nini tufanye ili watu wafaidike zaidi? Kuna hayo na mwengine ya kumwaga katika maongezi yetu haya, na yangu matumaini utamfahamu zaidi Christine na kumpa heshima yake anayostahili. Tafadhali enjoy.

Love,

Salama.



Follow:

Twitter: http://twitter.com/YahStoneTown

Instagram: http://Instagram.com/YahStoneTown

Facebook: http://facebook.com/YahStoneTown


---

Support this podcast: https://podcasters.spotify.com/pod/show/yahstonetown/support

1 hr 7 min