1 hr 4 min

Ep. 31 - Salama Na GOODLUCK | WASTAHILI SIFA Salama Na

    • Entertainment News

Sifa za Bwana inabidi zisemwe kwa zawadi hii alotupa sisi wanadamu, tunamshkuru sana kwa kipaji cha Goodluck Gosbert na tunamshkuru pia kwa kumfanya ni wa kwetu, kutoka nchini kwetu, kwamba ni mwenzetu. Kwa kweli binafsi nimependa sana na najivunia yeye.

Utamu wa sauti yake nadhani cha kwanza wengi tulikipenda sana, baada ya kumsikia tu, kama ilivyokua mara ya kwanza anataka kujifunza kupiga gitaa akaenda kanisani, na akaskika akiimba na wana kwaya wa kanisa hilo na wakampenda toka siku hiyo mpaka leo, ndo ilivyokua kwetu pia naamini. Kipaji chake cha pili ni utajiri wa mashairi, kipaji kikubwa cha kuandika na wakati naongea nae alitaja baadhi ya nyimbo kubwa alizowahi kuandika ambazo ni za ‘kidunia’ na pia kama zilimtia matatani kiasi maana imekua ikileta tafsiri nyengine kwa baadhi ya watu ambao wao wanamuona kwenye njia nyengine. Lakini hutunga nyimbo zake mwenyewe na pia anawaandikia wengine na katika hizo zinajumuisha kazi zake za nzuri tu alizowahi kufanya ambazo zilitufanya mimi na wewe tumkubali.

Kutoka kuwa mtoto pekee wa kiume nyumbani, na pia kukuzwa na Mama tu ambaye kwa mujibu wa Goodluck alikua muhangaikaji haswa, alifanya kila aliloweza kwa kujituma kuhakikisha watoto wake wanapata elimu ili ije kuwasaidia baadae lakini pia kukua kwenye maadili yaliyo bora kwa kumpenda na kumtanguliza Mungu. Mama yake hakuamini siku ya kwanza alipojua mtoto wake ni amejiunga na kwaya ya kanisani kwake. Na yaliyofuata baada ya hapo ni historia tu. Ungana nami kumskiliza Goodluck hapa na kama ilivyo kawaida, natumai utapata mawili matatu ya kukusogeza katika maisha yako. Tafadhali enjoy.

Love,

Salama.



Follow:

Twitter: http://twitter.com/YahStoneTown

Instagram: http://Instagram.com/YahStoneTown

Facebook: http://facebook.com/YahStoneTown


---

Support this podcast: https://podcasters.spotify.com/pod/show/yahstonetown/support

Sifa za Bwana inabidi zisemwe kwa zawadi hii alotupa sisi wanadamu, tunamshkuru sana kwa kipaji cha Goodluck Gosbert na tunamshkuru pia kwa kumfanya ni wa kwetu, kutoka nchini kwetu, kwamba ni mwenzetu. Kwa kweli binafsi nimependa sana na najivunia yeye.

Utamu wa sauti yake nadhani cha kwanza wengi tulikipenda sana, baada ya kumsikia tu, kama ilivyokua mara ya kwanza anataka kujifunza kupiga gitaa akaenda kanisani, na akaskika akiimba na wana kwaya wa kanisa hilo na wakampenda toka siku hiyo mpaka leo, ndo ilivyokua kwetu pia naamini. Kipaji chake cha pili ni utajiri wa mashairi, kipaji kikubwa cha kuandika na wakati naongea nae alitaja baadhi ya nyimbo kubwa alizowahi kuandika ambazo ni za ‘kidunia’ na pia kama zilimtia matatani kiasi maana imekua ikileta tafsiri nyengine kwa baadhi ya watu ambao wao wanamuona kwenye njia nyengine. Lakini hutunga nyimbo zake mwenyewe na pia anawaandikia wengine na katika hizo zinajumuisha kazi zake za nzuri tu alizowahi kufanya ambazo zilitufanya mimi na wewe tumkubali.

Kutoka kuwa mtoto pekee wa kiume nyumbani, na pia kukuzwa na Mama tu ambaye kwa mujibu wa Goodluck alikua muhangaikaji haswa, alifanya kila aliloweza kwa kujituma kuhakikisha watoto wake wanapata elimu ili ije kuwasaidia baadae lakini pia kukua kwenye maadili yaliyo bora kwa kumpenda na kumtanguliza Mungu. Mama yake hakuamini siku ya kwanza alipojua mtoto wake ni amejiunga na kwaya ya kanisani kwake. Na yaliyofuata baada ya hapo ni historia tu. Ungana nami kumskiliza Goodluck hapa na kama ilivyo kawaida, natumai utapata mawili matatu ya kukusogeza katika maisha yako. Tafadhali enjoy.

Love,

Salama.



Follow:

Twitter: http://twitter.com/YahStoneTown

Instagram: http://Instagram.com/YahStoneTown

Facebook: http://facebook.com/YahStoneTown


---

Support this podcast: https://podcasters.spotify.com/pod/show/yahstonetown/support

1 hr 4 min