1 hr 10 min

Ep. 50 - Salama Na SUGU | UJIO WA UMRI Salama Na

    • Entertainment News

Turudi nyuma mwaka 1999 wakati nilipomaliza kidato cha nne kwahiyo nilikua sina mitkasi mingi zaidi ya kumkimbia Mama inapofika mchana ili niende kucheza zangu basketball pale Msasani kiwanja cha Pazi. Nlikua natokea zangu Mbagala Charambe nachukua zangu basi mappa Mbagala Rangi tatu then muunganisho unaendelea mpaka nafika zangu mazoezini, nilifanya urafiki na makonda na madereva weeengi kiasi kwamba nilikua ‘staff’ kwenye daladala nyingi, na huwezi kuamini nyingi pia nilikua nikiingia basi radio nlikua namiliki MIMI. Station gani tunaskiliza au tape gani tunaweka ili safari inoge na muziki. Nakumbuka jinsi ambavyo Sugu alikua anaikosha, anakosha nafsi yangu na ya abiria wote ambao walikua wanasafiri nasi basi moja. Chini ya miaka 18 ilikua inaongea na mimi haswam inanifanya nisitake kuwa yule binti ambale Sugu alikua namuongelea ASILAN! Mikononi mwa Polisi… Album kali kama Nje ya Bongo, Millenium, Muziki na Maisha zilifuata na wakati hizi nyengine zinatoka nami tayari nilishaacha kumtia wasiwasi Mama yangu wa kurudi nyumbani usiku na kuwa DJ wa muda ndani ya Daladala za Mbagala Posta au Mbagala Kariakoo na kuweza kupata kazi yangu ya kwanza pale Times FM kabla sijajiunga na EA Radio na TV.

Mapenzi yangu kwa Sugu na muziki wake yako wazi na naamini na yeye anajua maana huwa namuambia kila tunapokutana, pia napenda kuwa around na yeye maana confidence yake ni kitu cha kujifunza. Haogopi, anajiamini na uthubutu wake katika mambo yake mengi ni jambo ambalo wengi wetu tunajifunza sana kutoka kwake. Kuanzia jinsi alivyokua anajibeba, mapinduzi ya uandishi na muziki ambayo amefanya na anaendelea kufanya mpaka leo hii ni kitu ambacho kama utakua unamfuatilia kwa karibu basi utakua huna la kufanya zaidi ya kupenda jinsi anavyofanya mambo yake.

Siku zote nimekua nikitaka saaana kufanya nae interview lakini kama tujuavyo, Mungu ndo mpangaji wa yote na round hii ilikua ndo wakati muafaka. Nilimcheki naye akakiambia kwamba Mimi ni mtu pekee ambaye angependa aongee naye so mengine yakawa historia tu.

Brother alikuja Dar es Salaam malum kabisa kwaajili ya kuongea na sisi na kwa hilo tunamshkuru sana. Mambo ya kisiasa yalikua sio focus yetu hata kidogo na badala yake tulitaka kumfahamu yeye zaidi na pengine mmoja anaweza kujifunza kwa kufuatilia tu nyenendo zake kwenye mitandao.

Kaka alishawahi kwenda jela, amempoteza Mama yake kipenzi pia muda si mrefu baada ya yeye kutoka. Sisi tuliongea naye kuhusu mapenzi yake na Mama yake kipenzi Desderia ambaye hata jina la hoteli yake ameipa jina la Mama yake. Nilitaka kujua ukaribu wao huo ulitokana na nini, jinsi ambavyo Mama alimpa support kipindi hicho ambacho muziki ulikua unaonekana kama uhuni tu. Maoni yake kwenye masuala mbali mbali na kuhusu urafiki na mafanikio. Pia nilitaka kujua historia yake ya muziki na njia alizowahi kupita. Mambo mengine ni kuhusu suala la yeye kuwa Baba na mapenzi kwa ujumla.

Yangu matumaini una enjoy maongezi haya na Kaka mkubwa na pia confidence yake kwenye masala mbalimbali itakufanya pia ujibebe kuelekea mbele!

Tafadhali enjoy.

Love,
Salama


---

Support this podcast: https://podcasters.spotify.com/pod/show/yahstonetown/support

Turudi nyuma mwaka 1999 wakati nilipomaliza kidato cha nne kwahiyo nilikua sina mitkasi mingi zaidi ya kumkimbia Mama inapofika mchana ili niende kucheza zangu basketball pale Msasani kiwanja cha Pazi. Nlikua natokea zangu Mbagala Charambe nachukua zangu basi mappa Mbagala Rangi tatu then muunganisho unaendelea mpaka nafika zangu mazoezini, nilifanya urafiki na makonda na madereva weeengi kiasi kwamba nilikua ‘staff’ kwenye daladala nyingi, na huwezi kuamini nyingi pia nilikua nikiingia basi radio nlikua namiliki MIMI. Station gani tunaskiliza au tape gani tunaweka ili safari inoge na muziki. Nakumbuka jinsi ambavyo Sugu alikua anaikosha, anakosha nafsi yangu na ya abiria wote ambao walikua wanasafiri nasi basi moja. Chini ya miaka 18 ilikua inaongea na mimi haswam inanifanya nisitake kuwa yule binti ambale Sugu alikua namuongelea ASILAN! Mikononi mwa Polisi… Album kali kama Nje ya Bongo, Millenium, Muziki na Maisha zilifuata na wakati hizi nyengine zinatoka nami tayari nilishaacha kumtia wasiwasi Mama yangu wa kurudi nyumbani usiku na kuwa DJ wa muda ndani ya Daladala za Mbagala Posta au Mbagala Kariakoo na kuweza kupata kazi yangu ya kwanza pale Times FM kabla sijajiunga na EA Radio na TV.

Mapenzi yangu kwa Sugu na muziki wake yako wazi na naamini na yeye anajua maana huwa namuambia kila tunapokutana, pia napenda kuwa around na yeye maana confidence yake ni kitu cha kujifunza. Haogopi, anajiamini na uthubutu wake katika mambo yake mengi ni jambo ambalo wengi wetu tunajifunza sana kutoka kwake. Kuanzia jinsi alivyokua anajibeba, mapinduzi ya uandishi na muziki ambayo amefanya na anaendelea kufanya mpaka leo hii ni kitu ambacho kama utakua unamfuatilia kwa karibu basi utakua huna la kufanya zaidi ya kupenda jinsi anavyofanya mambo yake.

Siku zote nimekua nikitaka saaana kufanya nae interview lakini kama tujuavyo, Mungu ndo mpangaji wa yote na round hii ilikua ndo wakati muafaka. Nilimcheki naye akakiambia kwamba Mimi ni mtu pekee ambaye angependa aongee naye so mengine yakawa historia tu.

Brother alikuja Dar es Salaam malum kabisa kwaajili ya kuongea na sisi na kwa hilo tunamshkuru sana. Mambo ya kisiasa yalikua sio focus yetu hata kidogo na badala yake tulitaka kumfahamu yeye zaidi na pengine mmoja anaweza kujifunza kwa kufuatilia tu nyenendo zake kwenye mitandao.

Kaka alishawahi kwenda jela, amempoteza Mama yake kipenzi pia muda si mrefu baada ya yeye kutoka. Sisi tuliongea naye kuhusu mapenzi yake na Mama yake kipenzi Desderia ambaye hata jina la hoteli yake ameipa jina la Mama yake. Nilitaka kujua ukaribu wao huo ulitokana na nini, jinsi ambavyo Mama alimpa support kipindi hicho ambacho muziki ulikua unaonekana kama uhuni tu. Maoni yake kwenye masuala mbali mbali na kuhusu urafiki na mafanikio. Pia nilitaka kujua historia yake ya muziki na njia alizowahi kupita. Mambo mengine ni kuhusu suala la yeye kuwa Baba na mapenzi kwa ujumla.

Yangu matumaini una enjoy maongezi haya na Kaka mkubwa na pia confidence yake kwenye masala mbalimbali itakufanya pia ujibebe kuelekea mbele!

Tafadhali enjoy.

Love,
Salama


---

Support this podcast: https://podcasters.spotify.com/pod/show/yahstonetown/support

1 hr 10 min