100 episodes

Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu United Nations

    • News
    • 5.0 • 5 Ratings

Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

    Simulizi ya kijana mkimbizi Gad Harindimana Mnyarwanda nchini Uganda - FAO inavyofungua uwezo

    Simulizi ya kijana mkimbizi Gad Harindimana Mnyarwanda nchini Uganda - FAO inavyofungua uwezo

    Makala inatupeleka nchini Uganda kumsikiliza Gad Harindimana, kijana mkimbizi kutoka Rwanda anayeishi katika makazi ya wakimbizi Nakivale mnufaika wa programu ya Huduma za Ajira Vijijini inayoungwa mkono na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi Duniani, ILO kupitia shirika lisilo la kiserikali la AVSI Foundation. Gad Harindimana amepata kazi ya ufundi pikipiki baada ya kukamilisha programu ya Huduma hizo. Anasimulia kwa lugha ya Kinyakole inayotafsiriwa na Anold Kayanda. 

    FAO waeleza kwa nini kuzuia upotevu na utupaji wa chakula ni muhimu na jukumu la kila mtu

    FAO waeleza kwa nini kuzuia upotevu na utupaji wa chakula ni muhimu na jukumu la kila mtu

    Katika siku ya kimataifa ya uhamasishaji kuhusu uelewa wa Upotevu na utupaji wa chakula, shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO linataka kila mtu atambue ni kwanini kuzuia na kupumguza upotevu na utupaji wa chakula ni muhimu hasa katika kuchangia mabadiliko ya mifumo ya chakula na utimizaji wa malengo ya maendeleo endelevu SDGs. 
    Siku yam waka huu ambayo imebeba mauadhui “Komesha upotevu na utupaji wa chakula kwa ajili ya watu na sayari” inaadhimishwa huku kati ya watu milioni 691 na 783 walikabiliwa na njaa mmwaka 2022 limesema shirika hilo.
    Likisisitiza jinsi hali inavyohitaji kubadilika haraka shirika hilo linasema wakati njaa na kutokuwa na uhakika wa chakula kukiendelea duniani mwaka 2022 inakadiriwa kuwa asilimia 13 ya chakula duniani ilipotea kwenye mnyororo wa thamani kuanzia baada ya kuvunwa na kabla ya kufika sokoni, na asilimia 17 nyingine ilitupwa majumbani, kwenye sehemu za utoaji huduma za chakula na kwenye masoko ya chakula.
    Hivyo FAO inatatoa mwito wa kuchukua hatua kwa mashirika ya umma, sekta binafsi, na kila mtu ili kupunguza upotevu na utupaji wa chakula (FLW) na kuelekea kubadilisha mifumo ya kilimo kwa ajili ya kuweza kuchangia katika mafanikio ya utekelezaji wa ajenda ya maendeleo ya 2030. 
    Kwani limesema Kupunguza upotevu na utupaji wa chakula kunaweza kuwa na jukumu muhimu katika sio tu kwa mabadiliko ya mifumo ya chakula ya kilimo bali pia kwa kuongeza upatikanaji wa chakula, kuchangia uhakika wa chakula, lishe bora, na kujenga mnepo. 
    Upunguzaji wa upotevu na utupaji wa chakula kwa mujibibu wa FAO pia hutumika kama mkakati muhimu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kwa kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi (GHGs). 
    Kwa hivyo unaweza kusaidia nchi na biashara kuongeza hamasa ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi, huku zikihifadhi na kulinda mifumo yetu ya ikolojia na maliasili ambayo mustakabali wa chakula huitegemea.
    FAO inasema hivi sasa, mifumo mingi ya kilimo ya chakula duniani sio endelevu, kwani inaharibu ardhi ya kilimo, inachangia uzalishaji wa gesi chafu na upotevu wa bioanuwai na hutumia maji mengi ya ardhini. 
    Mifumo ya chakula pia iko hatarini kwa majanga ya hali ya hewa na mishtuko mingine, kwa sababu ya athari kwa mazingira.

    29 SEPTEMBA 2023

    29 SEPTEMBA 2023

    Hii leo jaridani tunaangazia utupaji wa chakula, na uchaguzi ujao nchini Sudan Kusini. Makala tunakupeleka nchini Uganda na mashinani nchini DRC, kulikoni?.
    Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York, Marekani, Baraza la Usalama limejadili hali ya kibinadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambapo awali Naibu Mkuu wa ofisi ya Umoja huo kuhusu misaada ya kiutu Joyce Msuya anataja changamoto zinazokumba taifa hilo.Wakati nchi ya Sudan Kusini ikijiandaa kushiriki katika uchaguzi mkuu kwa mara ya kwanza kabisa tangu ipate uhuru, Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNMISS unaendesha makongamano na vyama vya siasa nchini humo.Makala inatupeleka nchini Uganda kumsikiliza Gad Harindimana, kijana mkimbizi kutoka Rwanda anayeishi katika makazi ya wakimbizi Nakivale mnufaika wa programu ya Huduma za Ajira Vijijini inayoungwa mkono na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi Duniani, ILO kupitia shirika lisilo la kiserikali la AVSI Foundation. Harindimana anasimulia kwa lugha ya Kinyakole inayotafsiriwa na Anold Kayanda.Katika mashinani tutammsikia mwanamke ambaye aliweza kujifungua salama, na bila malipo, kwa usaidizi wa wakunga katika kliniki tembezi inayohifadhiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya watu, UNFPA katika kambi ya wakimbizi wa ndani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC.Mwenyeji wako ni Assumpta, karibu!

    UNMISS wataka wanasiasa Sudan Kusini wapatie wanachi elimu ya kisiasa

    UNMISS wataka wanasiasa Sudan Kusini wapatie wanachi elimu ya kisiasa

    Wakati nchi ya Sudan Kusini ikijiandaa kushiriki katika uchaguzi mkuu kwa mara ya kwanza kabisa tangu ipate uhuru, Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNMISS unaendesha makongamano na vyama vya siasa nchini humo. 
    Ikiwa imesalia miezi 15 mpaka uchaguzi ufanyike hapo Desemba 2024 UNMISS wanasema lengo la kuandaa makongamano hayo nikujenga utamaduni wa kuwa na mazungumzo thabiti, kutatua changamoto zinazowakabili kuhusu utawala bora na kujenga kuaminiana miongoni mwa wanasiasa na jamii wanazozitumikia. 
    Akiwa katika moja ya majukwaa huyo katika mji mkuu wa Juba Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini ambaye pia ni Mkuu wa UNMISS, Nicholas Haysom aliwaambia washiriki kuwa, “Uchaguzi hauwezi kufanyika ikiwa hakuna makubaliano ya masuala ya kiufundi. Hisia za uharaka walizonazo jumuiya ya kimataifa kuhusu uchaguzi hazisaidii. Udharura unawahusu Wasudan Kusini — wananchi, na hasa vyama vya siasa, ndiyo maana tutawaomba nyinyi kufanya kazi na kutusaidia sisi katika kuunda na kuelewa asili ya chaguzi mnazotaka kufanya ili na sisi tuweze kuhamasisha kupatikana kwa misaada kwa ajili ya mambo hayo.”
    Si wanasiasa pekee wanaohudhuria makongamano hayo bali pia wasomi ambao wamehimiza umuhimu wa kuwa na ushiriki mkubwa wa umma katika michakato ya amani, pamoja vyama vya siasa kuwa na ushindani imara kama anavyoeleza Adwak Nyaba, “Vyama vya siasa vinapaswa kuhimiza elimu ya kisiasa ili kuongeza ufahamu wa kijamii na ufahamu wa kisiasa wa wananchi. Ni kutokana na kuwepo kwa ufahamu wa kisiasa na watu wanaozingatia siasa kunakowezesha uwepo wa serikali za kidemokrasia. Ikiwa watu hawana ufahamu kabisa wa kisiasa, huwezi kuzungumzia utawala wa kidemokrasia, au huwezi kuzungumzia demokrasia.”
    Wanasiasa wamehimizwa kufikia makubaliano ya masuala muhimu haswa kuhusu uanzishwaji wa taasisi muhimu ambazo ni Baraza la Vyama vya Siasa, Tume ya Kitaifa ya Marekebisho ya Katiba na Tume ya Kitaifa ya Uchaguzi.

    Methali: Umekuwa Jeta Hubanduki!

    Methali: Umekuwa Jeta Hubanduki!

    Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mkuu wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anachambua methali Umekuwa Jeta Hubanduki! 

    28 SEPTEMBA 2023

    28 SEPTEMBA 2023

    Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO nchini Tanzania kwa kushirikiana na wadau wake wamewezesha hatua ya upimaji wa udongo katika wilaya sita ambako mradi wa kulinda na kuhifadhi baiyonuai unatekelezwa. Kazi hiyo imefanywa na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine - SUA, na sasa utafiti huo umekamilika, Je umebaini nini? John Kabambala wa redio washirika KidsTime ya Morogoro-Tanzania amehudhuria uzinduzi wa ripoti hiyo ya vipimo vya udongo. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za ulinzi wa amani, haki za binadamu na ubaguzi wa rangi. Na katika kujifunza lugha ya kiswahili tunakuletea maana ya methali “UMEKUWA JETA HUBANDUKI”.
    Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York, Marekani, Baraza la Usalama limejadili hali ya kibinadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambapo awali Naibu Mkuu wa ofisi ya Umoja huo kuhusu misaada ya kiutu Joyce Msuya anataja changamoto zinazokumba taifa hilo.Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu Volker Türk, ametoa wito wa ujumbe wa kimataifa wa kusaidia polisi wa kitaifa nchini Haiti kutokomeza mzunguko wa ghasia uliojikita kwenye ngazi zote za jamii na kuchochea janga la ukosefu wa usalama na haki za binadamu.Na mfumo wa kibaguzi dhidi ya wamarekani weusi wenye asili ya Afrika umepenyezwa hadi kwenye utendaji wa jeshi la polisi na mfumo wa mahakama nchini Marekani na hivyo lazima marekebisho ya haraka yafanywe ili kuondokana na madhila yanayokumba wananchi hao, imesema ripoti mpya ya wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mkuu wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anachambua methali “Umekuwa Jeta Hubanduki!”.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Customer Reviews

5.0 out of 5
5 Ratings

5 Ratings

Top Podcasts In News

The New York Times
NPR
Strike Force Five
The Daily Wire
The Daily Wire
Cumulus Podcast Network | Dan Bongino

More by United Nations

United Nations
United Nations
United Nations
United Nations
United Nations
United Nations