The Uongozi Wa Kiroho Podcast uongoziwakiroho
-
- Religion & Spirituality
Ushauri wa kiutendaji na mafundisho ya kibiblia kusaidia kukidhi mahitaji ya Viongozi wa Kiroho
-
Tulee Wengine Wawe Nasi Katika Uongozi
Mchungaji Cyprian Michael anatushauri juu ya uongozi wa familia na uongozi kanisani katika podcast hii. Badala ya kuongoza tukiwa peke yetu, anatuhimiza kulenga watu wenye sifa na uwezo wa kuongoza na kuwaandaa ili wawe bega kwa bega pamoja nasi katika uongozi na wawe tayari kushika uongozi wa huduma siku zijazo.
-
Tufanye Uanafunzi!
Mchungaji Emmanuel Mwankasole kutoka Dodoma, Tanzania anatukumbusha juu ya umuhimu wa kufanya uanafunzi. Baada ya kujibu swali la msingi "Kwa nini tufanye?" yeye anaendelea kutoa mafunzo mazuri sana kwa ajili ya viongozi, namna ya kufanya uanafunzi na faida tutakazoziona tukifanya uanafunzi kwa uaminifu. Bila shaka utabarikiwa na kujengwa na podcast hii.
-
Afya Ya Kiroho
Kiongozi D. Kitang'wa anatushauri kuhusu afya katika mwili wa Kristo. Ili afya ya kiroho iwe nzuri, inabidi sisi tulio viongozi wa kiroho tufundishe watu wetu vizuri. Haitoshi tu kuwafundisha kuepukana na dhambi ambazo zimekatazwa na Mungu katika Neno lake, lakini tunapaswa kuwafundisha kutii na kutenda tuliyoamriwa naye vilevile.
-
Kanuni Muhimu - Seh. 1
Sisi sote tuna mawazo yetu juu ya kanisa na uongozi katika kanisa, lakini mawazo yetu siyo sawa. Ni kwa sababu tumeathiriwa na mila na utamaduni pamoja na uzoefu wetu tangu utoto. Kuna aina mbalimbali za makanisa na namna tofauti tofauti za uongozi katika kanisa. Je, zote zinakubalika? Zote ni za kibiblia? Podcast hii na zingine zifuatazo zitahusu mada hii ya kanuni muhimu kutoka Neno la Mungu zinazotuongoza tuwe na kanisa la kibiblia na uongozi unaokubaliwa na Bwana.
-
Kulea Viongozi Wengine
Mzee Smith anazungumza na mchungaji ambaye, pamoja na kuongoza kanisa na kufanya huduma nyingine nyingi, anaweka mkazo katika kazi muhimu ya kulea viongozi wengine. Sikiliza mashauri yake namna ya kutambua viongozi wa siku zijazo na jinsi ambavyo mchungaji anaweza kuwafundisha na kuwalea katika kanisa.
-
Mauti Imemezwa
Tunapoomboleza kifo cha ndugu zetu, viongozi wenzetu, hebu tukumbuke mambo haya.