Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu United Nations
-
- News
-
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
-
LANDESA yaelezea ni vipi ushiriki wao CSW68 unaleta nuru kwa wanawake Tanzania
Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ukiendelea hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa imeendelea kuzungumza na washiriki ili kufahamu yale wanayofanya kutekeleza maudhui ya kipaumbele ya mwaka huu ya kumwezesha mwanamke na mtoto wa kike ili hatimaye kupunguza umaskini na kuimarisha usawa wa kijinsia. Shirika la kiraia la kutetea haki ya ardhi kwa wanawake, LENDESA tawi la Tanzania linaloungwa mkono na shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia masuala ya wanawake ni miongoni mwa washiriki ambapo Assumpta Massoi wa Idhaa hii amezungumza na Khadija Mrisho, anayeongoza kampeni ya kimataifa ya Linda Ardhi ya Mwanamke au Stand For Her Land. Khadija anaanza na kile kilichowaleta.
-
FAO: Baa la njaa lanyemelea Gaza
Hali ya uhakika wa kupata chakula huko Gaza, ni tete na baa la njaa linanyemelea kwenye majimbo ya kaskazini mwa eneo hilo imesema ripoti mpya ya hali ya chakula Gaza iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, likisema jawabu la kuondokana na hali hiyo ni amani.
Rein Paulsen, Mkurugenzi wa Ofisi ya Masuala ya Dharura na Mnepo FAO akizungumza hii leo huko Roma, Italia wakati wa kutolewa kwa ripoti hiyo ya uchambuzi wa viwango vya uhakika wa kupata chakula au IPC kwa Ukanda wa Gaza, anasema takwimu zinajenga taswira ya hali ya kutia wasiwasi mkubwa. Na pindi tunapofikiria kuhusu Gaza Kaskazini, ambako hali ni mbaya zaidi, uchambuzi wa sasa unatuonesha kuwa njaa ni dhahiri katika kipindi cha kuanzia sasa na Mei 2024.
Hii ina maana tunapotazama mwelekeo wa takwimu za hali ya upatikanaji chakula na lishe tunaona hali ya kutisha. Kusini, hali nayo imezidi kuwa mbaya na huko tunashikilia makadirio yetu ya uwezekano wa baa la njaa.”
Ripoti inaonesha kuwa mwendelezo wa uhasama umesambaratisha sekta ya kilimo, ambayo familia za Gaza inategemea kwa ajili ya kujipatia kipato.
“Watu wote kwenye ukanda wa Gaza wanakabiliwa na viwango vya juu vya ukosefu mkubwa wa chakula ukiwekwa katika kiwango cha 3, na 4. Hii inaamanisha nusu ya idadi ya watu wote wa eneo hilo, takribani milioni 1.1 wanaweza kukabiliwa na janga kubwa la ukosefu wa uhakika wa chakula la kiwango cha 5.”
Hivyo amesema usaidizi wa haraka unahitajika kurejesha uzalishaji wa chakula na kwa mujibu wa ripoti
“Inatueleza kuwa baadhi ya mifugo iko hai, na inaweza kusaidiwa na ndio maana FAO inajikita kusaidia mahitaji ya kujipatia kipato Ukanda wa Gaza. Kwa sasa tumepata kibali cha kupeleka tani 1500 za ujazo za chakula cha mifugo.”
Amesema uhai wa mifugo utakuwa hakikisho la upatikanaji wa maziwa kwa familia, maziwa ambayo yatakuwa ni lishe bora kwa watoto na hivyo kukabili utapimlo uliokithiri miongoni mwa watoto.
Akatamatisha akisema, “uhakika wa kupata chakula utawezekana kukiweko na amani. Na haki ya kupata chakula ni haki ya msingi. Hili linapaswa kuzingatiwa na wadau wote.” -
18 MACHI 2024
Hii leo jaridani tunaangazia baa la njaa unalowakumba waPalestina katika ukanda wa Gaza, na kesi zinazohusisha wanajeshi wa nchi ya Sudan Kusini. Makala tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa, na mashinani tunakupeleka nchini Kenya, kulikoni?
Hali ya uhakika wa kupata chakula huko Gaza, ni tete na baa la njaa linanyemelea kwenye majimbo ya kaskazini mwa eneo hilo imesema ripoti mpya ya hali ya chakula Gaza iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, likisema jawabu la kuondokana na hali hiyo ni amani.Timu kutoka Kurugenzi ya Haki na Sheria ya Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Sudan Kusini (SSPDF) mwishoni mwa wiki kwa usaidizi wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), imehitimisha tathmini yake katika Kaunti ya Maridi jimboni Equatorial Magharibi kutathmini kesi zinazohusisha wanajeshi wa nchi hiyo. Assumpta Massoi wa Idhaa hii akizungumza na Khadija Mrisho, Afisa kutoka shirika la kiraia la kutetea haki ardhi kwa mwanamke LANDESA tawi la Tanzania yeye akiwa kiongozi wa kampeni ya kimataifa ya Linda Ardhi ya Mwanamke. Akiwa hapa New York, Marekani akishiriki mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68, anaelezea kile walichojifunza. Lakini anaanza na kile kilichowaleta.Katika mashinani tutaelekea Ngong nchini Kenya kusikia ujumbe unaotia moyo wasichana waathirika wa mimba za utotoni.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! -
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wasaidia jeshi la Sudan Kusini kutathmini kesi dhidi ya askari
Timu kutoka Kurugenzi ya Haki Sheria ya Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Sudan Kusini (SSPDF) mwishoni mwa wiki kwa usaidizi wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), imehitimisha tathmini yake katika Kaunti ya Maridi jimboni Equatorial Magharibi kutathmini kesi zinazohusisha wanajeshi wa nchi hiyo.
Tathimini itawezesha kufunguliwa mashtaka kwa askari wa jeshi ambao wanashukiwa kufanya uhalifu mkubwa, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa kingono na aina nyingine za unyanyasaji wa kijinsia.
Mama Sarah Bennert, mwanaharakati na mwakilishi wa wanawake anasema hatua hii inawakilisha ishara ya haki na uwajibikaji.
"Tuna masuala mengi yanayotukabili hapa kama wanawake. Wakati mwingine unaripoti kesi na haki imechelewa na unabaki kukata tamaa na bila msaada wowote. Sasa, kwa uwepo wa timu ya tathmini hapa chini tunatumai kesi hizo zote walizozizingatia zitasikilizwa kwa sababu baadhi yetu ambao bado tuna kesi tuna kiwewe."
Idrissa Sylvaine ni Mshauri wa haki sheria wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS) anasema,
“Tathmini hiyo itasaidia kukuza utawala wa sheria, kuleta haki kwa waathiriwa na kuwawajibisha askari wa SSPDF. Tathmini hiyo pia itachangia katika mchakato wa amani nchini Sudan Kusini.” -
Ushirkiano wa dhati waliotuonesha ulifanya wananchi waachane na mpango wa kuwapiga mawe MONUSCO- Chifu Makofi
Hii leo huko jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kikosi cha 10 cha Tanzania (TANZBATT-10) kilichoko kwenye brigedi ya mapigano (FIB) ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO imekabidhi majukumu kwa kikosi cha 11, TANZBATT-11, katika hafla iliyofanyika eneo la Beni-Mavivi. Msimulizi wetu ni Kapteni Abubakari Muna, Afisa Habari wa TANZBATT-10.
Mkuu wa TANZBATT-10 Luteni Kanali John Peter Kalabaka amekabidhi bendera ya Tanzania kwa Kamanda wa TANZBATT-11 Luteni Kanali Vedasto Ernest Kikoti ikiwa ni ishara ya kuanza majukumu ya ulinzi wa amani, katika tukio ambalo mgeni rasmi alikuwa Kaimu Kamanda wa FIB-MONUSCO Kanali Alex Tamson Malenda.
Akizungumza kwenye hafla hiyo Luteni Kanali Kalabaka amesema kwenye upande wa operesheni wameweza kukabili na kupunguza mashambulizi yanayofanywa na vikundi vilivyojihami kwenye eneo la ulinzi la TANZBATT-10 halikadhalika kuepusha mauaji ya raia wasio na hatia na pia kuepusha vitendo vya ubakaji.
“Kijamii tumeweza kushirikiana na jamii ya hapa Beni-Mavivi na pia kuwapatia misaada mbali mbali ya kijamii,” amesema Mkuu huyo wa TANZBATT-10.
Luteni Kanali Vedasto Ernest Kikoti ambaye amepokea jukumu la ulinzi akaeleza bayana kuwa watatekeleza majukumu yao vyema kwa kuzingatia taratibu za Umoja wa Mataifa na kwamba watakuwa tayari kuendelea kushirikiana na raia.
“Tunaomba wananchi wakubali na waelewe dhamira hiyo, waukubali Umoja wa Mataifa ili kuupa nafasi uweze kutekeleza wajibu wake wa kulinda wananchi wa DRC,” ameeleza Luteni Kanali Kikoti.
Makofi Bukuka Gervain ambaye ni Chifu wa eneo hilo akashukuru TANZBATT-10 kwa ushirikiano walioonesha wakati wote wa kipind ichao cha ulinzi wa amani Beni-Mavivi na kueleza kuwa Kamanda wa Kikosi hicho alikuwa yuko karibu sana na wanajamii akitolea mfano wakati wa michezo ikiwemo mpira wa miguu.
“Ushirikiano wao na sisi umewezesha raia kufungua nyoyo zao na kuondokana na fikra zao za kupiga mawe MONUSCO barabarani. Sasa barabara zilibaki wazi na MONUSCO wakafanya kazi yao vema,” amesema Chifu Makofi
Meja Fatuma Haruna Makula, wa TANZBATT-11 ameahidi kuendeleza uhusiano mzuri kati ya wanajeshi wanawake kutoka Tanzania na wanawake wa Beni-Mavivi akisema, “wanawake maafisa na askari tuliokuja hapa wote tumepita mafunzo mbali mbali kuhusu suala zima la ulinzi wa amani. Tutahakikisha wanashiriki vema shughuli za ulinzi wa mani kwa mujibu wa taratibu za Umoja wa Mataifa chini ya MONUSCO.”
Imeandaliwa na Luteni Abubakari Muna, Afisa Habari, TANZBATT-10
TAGS: Amani na Usalama
News: TANZBATT 10, TANZBATT-11
REgion.: Afrika
Focus: DRC
UN/Partner: MONUSCO -
Wasichana ni majaji watarajiwa, wafuate ndoto zao katika masomo ya Uanasheria - Hakimu Pamela Achieng
Maadhimisho ya kwanza ya Siku ya Majaji Wanawake duniani yalifanyika tarehe 10 Machi 2022, ikiangazia Haki katika Mtazamo wa Kijinsia. Umoja wa Mataifa umeendelea kuadhimisha siku hii kama sehemu ya juhudi za kimataifa za kuhakikisha usawa wa kijinsia na kushughulikia masuala ya uadilifu wa mahakama yanayohusiana na jinsia. Huku mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ukiendelea hapa jijini New York Marekani, nchini Kenya Selina Jerobon wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kupitia video iliyoandaliwa na washirika wetu Redio Domus amekutana na Pamela Achieng, Hakimu katika mahakama ya Ngong iliyo katika Kaunti ya Kajiado ambaye anaanza kwa kuelezea ni kwa nini kama mwanamke aliamua kuingia katika tasnia hii.