11 episodes

Wahariri wetu wenye tajriba wanatoa hoja na mitazamo mizito kuhusu masuala yanayogonga vichwa vya habari, kila wiki.

Hoja za Wahariri The Standard Group PLC

    • News

Wahariri wetu wenye tajriba wanatoa hoja na mitazamo mizito kuhusu masuala yanayogonga vichwa vya habari, kila wiki.

    Vita vya Urusi na Ukraine; athari kwa dunia

    Vita vya Urusi na Ukraine; athari kwa dunia

    Mwanahabari mstaafu wa kimataifa, Abdu Mtullya anasema vita vya Urusi na Ukraine havistahili na huenda vikaathiri zaidi uchumi duniani, ikiwamo Afrika. Vita hivyo vimesababisha kupanda kwa bei ya mafuta, Urusi ikiendelea kurusha makombora katika ngome za Ukraine, hali ambayo haijawahi kushuhudiwa tangu mwaka wa 2014.

    • 7 min
    Mzozo wa Urusi na Ukraine; Mohamed Abdul-Rahman anachambua

    Mzozo wa Urusi na Ukraine; Mohamed Abdul-Rahman anachambua

    Je, unafahamu chimbuko la mgogoro kati ya Urusi na Ukraine, athari zake na unamaanisha nini kwa Afrika na dunia nzima? Mwanahabari/ Mhariri mstaafu na mchambuzi wa masuala ya kimataifa, Mohamed Abdul-Rahman anasimulia.

    • 14 min
    Hoja za Wahariri: Kitendawili cha mili Mto Yala - ndani ya magunia

    Hoja za Wahariri: Kitendawili cha mili Mto Yala - ndani ya magunia

    Dunia inazidi kushangazwa na suala la mili zaidi ya 20 kupatikana ndani ya magunia katika Mto Yala. Mili hiyo ina alama na ishara za mateso. Je, waliouliwa ni akina nani na sababu za kuuliwa ni gani? Aidha, twajadili siasa za OKA vilevile usajili wa wapigakura wapya. Ali Manzu anawashirikisha wanahabari, Shisia Wasilwa na Kennedy Wandera katika kudadavua masuala haya.

    • 43 min
    Hoja za Wahariri Podcast: Nchi bila umeme; ni njama?

    Hoja za Wahariri Podcast: Nchi bila umeme; ni njama?

    Kupotea kwa umeme nchini Kenya kwa takribani siku tatu kumechochea ghadhabu. Baadhi wanahisi kwamba ni njama ya wafanyakazi fulani wa kampuni za umeme kusababisha hali hiyo maksudi. Kwamba huenda wanalalamikia mageuzi ya usimamizi katika Kenya Power, ama ni kero la wasambazaji wa kawi kulalamikia viwango vipya vya ada za umeme ambavyo ni vya chini, na kuishia wao kupata hasara. Aidha, tunajadili kujiuzulu kwa Mshirikishi wa Utawala, Bonde la Ufa, George Natembeya ili kulenga kiti cha kisiasa. Ali Manzu anawashirikisha wahariri, Charles Otieno na Kennedy Wandera katika kuyajadili masuala haya.

    • 41 min
    Hoja za Wahariri Podcast: Ahadi za wanasiasa; watatekeleza?

    Hoja za Wahariri Podcast: Ahadi za wanasiasa; watatekeleza?

    Wagombea mbalimbali wa urais nchini Kenya wanazidi kutoa ahadi wanazosema watatekeleza endapo watashinda uchaguzi wa 2022. Katika podcast hii, wahariri Geoffrey Mung'ou, Roselyne Obala na mwanahabari mwandamizi, Mike Nyagwoka wanajadili iwapo ahadi zenyewe zinatekelezeka au la kwa kuweka kwenye mizani ahadi za sasa na za awali.

    • 12 min
    Hoja za Wahariri Podcast: Raila ni chaguo la Uhuru, huku siasa zikichacha Mlima Kenya

    Hoja za Wahariri Podcast: Raila ni chaguo la Uhuru, huku siasa zikichacha Mlima Kenya

    Rais Uhuru Kenyatta amewasihi wanasiasa wa One Kenya Alliance kumuunga mkono Raila Odinga kuelekea uchaguzi mkuu wa 2022, huku pendekezo lake likikataliwa vikali na wanasiasa hao. Aidha, wanasiasa mbalimbali wanazidi kujitokeza kwenye eneo la Mlima Kenya wakishindania udhibiti wa siasa za eneo hilo, Uhuru anapoelekea kustaafu. Je, kati ya William Ruto na Raila Odinga, ni nani atakayenufaika katika siasa za Mlima Kenya na ni nani atakayepoteza? Eneo la Mlima Kenya litaamua siasa za 2022? Wawaniaji wa urais wawateue wagombea wenza kutoka maeneo gani ya nchi? Mhariri, Geoffrey Mung'ou na wanahabari wa Standard - Chris Thairu na Mike Nyagwoka wanayapambanua masuala haya.

    • 26 min

Top Podcasts In News

The Daily
The New York Times
Serial
Serial Productions & The New York Times
Up First
NPR
The Tucker Carlson Show
Tucker Carlson Network
The Ben Shapiro Show
The Daily Wire
The Megyn Kelly Show
SiriusXM