1 min

Mashirika ya UN yaonya kuwa maelfu ya maisha ya watu El Fasher Sudan yako hatarini Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

    • Daily News

Mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa leo yameonya kwamba maisha ya maelfu ya watu yako hatarini El Fasher Sudan, kufuatia mashambulizi makali yanayoendelea ambapo moja ya hospitali Darfur Kaskazini imeshambuliwa na kukatili maisha ya watu wawili lakini pia kuchochea hofu ya kurejea kwa baa la njaa. 
Kwa mujibu wa Mratibu wa misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Martin Griffiths, “Shambulio hilo limeharibu paa la hospitali katika kituo cha huduma za dharura kwenye Hospitali ya Sourthen katika mji wa El Fasher ambayo ndio hospitali pekee inayofanyakazi kwas asa katika jimbo la Darfur Kaskazini na ambako vifaa vya matibabu na dawa sasa karibu vinakwisha.” 
Amesema takriban watu 800,000 wanaishi katika mji wa El Fasher na maelfu ya maisha yao yako hatarini huku taifa zima la Sudan likiwa katika hali mbaya.
Shirika la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA limesema makumi ya raia waliuawa mwishoni mwa wiki katika mapigano mapya  makubwa yaliyozuka Ijumaa kati ya vikosi vya serikali ya Sudan SAF na vikosi vya msaada wa haraka RSF katika eneo la Darfur Kaskazini ambalo ndilo lililosalia chini ya udhibiti wa serikali.
Shirika hilo linasema hivi sasa karibu watu milioni 25 nchini Sudan wanahitaji msaada wa kibinadamu na watu milioni 17.7 miongoni mwao wanakabiliwa na hali mbaya ya kutokuwa na uhakika wa chakula na kuna hofu kubwa ya kurejea kwa baa la njaa Darfur.
Nayo mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la luhudumia wakimbizi UNHCR na la uhamiaji IOM yamesema takriban watu 570,000 wametawanywa katika jimbo la Darfur Kaskazini katika miezi 13 iliyopita, wengine milioni 6.7 nchini Sudan ni wakimbizi wa ndani huku milioni 1.8 wamekimbilia katika nchi za jirani.

Mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa leo yameonya kwamba maisha ya maelfu ya watu yako hatarini El Fasher Sudan, kufuatia mashambulizi makali yanayoendelea ambapo moja ya hospitali Darfur Kaskazini imeshambuliwa na kukatili maisha ya watu wawili lakini pia kuchochea hofu ya kurejea kwa baa la njaa. 
Kwa mujibu wa Mratibu wa misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Martin Griffiths, “Shambulio hilo limeharibu paa la hospitali katika kituo cha huduma za dharura kwenye Hospitali ya Sourthen katika mji wa El Fasher ambayo ndio hospitali pekee inayofanyakazi kwas asa katika jimbo la Darfur Kaskazini na ambako vifaa vya matibabu na dawa sasa karibu vinakwisha.” 
Amesema takriban watu 800,000 wanaishi katika mji wa El Fasher na maelfu ya maisha yao yako hatarini huku taifa zima la Sudan likiwa katika hali mbaya.
Shirika la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA limesema makumi ya raia waliuawa mwishoni mwa wiki katika mapigano mapya  makubwa yaliyozuka Ijumaa kati ya vikosi vya serikali ya Sudan SAF na vikosi vya msaada wa haraka RSF katika eneo la Darfur Kaskazini ambalo ndilo lililosalia chini ya udhibiti wa serikali.
Shirika hilo linasema hivi sasa karibu watu milioni 25 nchini Sudan wanahitaji msaada wa kibinadamu na watu milioni 17.7 miongoni mwao wanakabiliwa na hali mbaya ya kutokuwa na uhakika wa chakula na kuna hofu kubwa ya kurejea kwa baa la njaa Darfur.
Nayo mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la luhudumia wakimbizi UNHCR na la uhamiaji IOM yamesema takriban watu 570,000 wametawanywa katika jimbo la Darfur Kaskazini katika miezi 13 iliyopita, wengine milioni 6.7 nchini Sudan ni wakimbizi wa ndani huku milioni 1.8 wamekimbilia katika nchi za jirani.

1 min

More by United Nations

UN News - Global perspective Human stories
United Nations
Noticias ONU - Mirada global Historias humanas
United Nations
联合国新闻 - 全球视野, 常人故事
United Nations
Interviews
United Nations
The Lid is On
United Nations
UNcomplicated
United Nations