Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

  1. 1 DAY AGO

    21 FEBRUARI 2025

    Hii leo jaridani tunaangazia mahitaji ya wakimbizi wanaokimbia machafuko DRC wakielekea nchini Burundi, na hali ya wakimbizi wa ndani Gaza wakati huu wa msimu wa baridi. Makala tunakurejesha nchini DRC na mashinani tunakwenda nchini Tanzania. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi, UNHCR limetoa ombi la dola milioni 40.4 ili kujiandaa na kutoa huduma za kuokoa maisha na usaidizi kwa wakimbizi wa ndani na waliokimbilia nchi jirani baada ya wakati huu ambapo mashambulizi ya waasi wa M23 yanazidi kufurusha raia kutoka Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokraia ya Congo, DRC.Huko Gaza Kaskazini, kwenye eneo la wapalestina linalokaliwa na Israeli, familia zilizofurushwa makwao kutokana na vita kati ya Israeli na wanamgambo wa Hamas wanavumilia msimu wa baridi kali katika makazi ya muda ya mahema yanayopigwa na upepo na mvua usiku na mchana, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF. Nyumba zao zimeharibika na kuacha watoto kuishi katika mazingira mabaya.Katika makala Evarist Mapesa anakupeleka eneo la mpakani mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, na Burundi kufuatilia mmiminiko wa wakimbizi kutoka DR Congo.Na mashinani fursa ni yake Regnihadah Mpete kutoka Tanzania ambaye anatumia kiswahili, lugha ya taifa nchini Tanzania kufundisha vikundi vya wanawake wilayani Biharamulo, mkoani Kagera jinsi ya kujikinga na magonjwa. Mafunzo serikali  kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani (UNICEF) kupitia TIP ambao ni Mtandao wa Madhehebu ya Dini mbalimbaliMwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

    11 min
  2. 1 DAY AGO

    Watoto watota kwa mvua katika ukanda Gaza, huku baridi kali ikitishia afya zao

    Huko Gaza Kaskazini, kwenye eneo la wapalestina linalokaliwa na Israeli, wanafamilia zilizofurushwa makwao kutokana na vita kati ya Israeli na wanamgambo wa Hamas wanavumilia msimu wa baridi kali katika makazi ya muda ya mahema yanayopigwa na upepo na mvua usiku na mchana, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF. Nyumba zao zimeharibika na kuacha watoto kuishi katika mazingira mabaya.  Ni sauti ya watoto wakitembea katikati ya mahema ya muda kwenye vichochoro vilivvyojubikwa na matope, hapa Gaza Kaskazini, huku wakijaribu kukwepa madimbwi ya maji yaliyosababishwa na mvua kubwa. Kupitia video iliyoandaliwa na UNICEF, Shahd Omar, msichana mwenye umri wa miaka kumi na saba, anaonekana amembeba nduguye, wengine wanaonekana wamekujikunyata kutokana na baridi. Shahd sasa akiwa amesimama nje hema lao anaelezea jinsi nyumba zao zilivyoharibiwa. “Tunavumilia hali ngumu sana,mvua kubwa, baridi, na upepo mkali, maisha ni magumu sana. Nyumba yetu ilivyoshambuliwa na kubomoka tulijitoa kwenye vifusi. Nyumba yetu imeharibika, hatuna samani, hakuna vituo vya kujikinga, wala mahali pa kukaa ili kupata joto. Maisha ni magumu. Hema letu lilikuwa karibu kupeperuka kwa sababu ya upepo mkali.” Kwingineko hapa, watoto wanaonekana wakicheza kwenye matope nje ya mahema zao huku maji yakitiririka kama mto. Layla Abu Asi ni mama wa watoto watatu, mwenye umri wa miaka 27 anasema, “Baridi hii ni kali mno, haiwezi kuvumilika ,upepo huu mkali umeleta madhara makubwa kwenye hema letu. Tangu asubuhi, maji ya mvua yamejaa kwenye hema letu, kila kitu kilichomo ndani kikilowa na kujaa maji. Watoto wangu wametota kwa maji ya mvua. Hii ni hali mbaya zaidi ambayo tumewahi kukumbana nayo.” UNICEF na wadau wanafanya kila wawezalo kuwasaidia wakazi wa Gaza.

    2 min

About

Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

More From United Nations

To listen to explicit episodes, sign in.

Stay up to date with this show

Sign in or sign up to follow shows, save episodes and get the latest updates.

Select a country or region

Africa, Middle East, and India

Asia Pacific

Europe

Latin America and the Caribbean

The United States and Canada