
12 episodes

Sheria Poa Podcast Privaty Rugambwa
-
- Education
-
-
5.0 • 2 Ratings
-
Sheria Poa, ni kipindi ambacho tunaongelea maswala mbalimbali ya jamii kwa mtazamo wa sheria na kwa lugha nyepesi kabisa na ya kiurafiki, ni kipindi cha kufundisha na kusaidia kwa watu wa aina zote.
-
The concept of Marital Rape: Time to amend our laws? (Suala la Ubakaji ndani ya ndoa: Je ni muda wa kurekebisha sheria zetu?)
Swala la ubakaji ndani ya ndoa; yaani mume kumbaka mke wake, ni tatizo kubwa sana duniani. Suala hili pia limekuwa likiwatokea wanandoa wengi sana Tanzania na hivyo kuibua maswali mengi sana juu ya sheria zetu katika suala hili, na wengi wamekuwa wakiuliza kama ndoa ni kibali au leseni ya kubaka (whether marriage is a licence to rape)
Kwenye mada hii leo tupo na Wakili Msomi Victor Mwakimi, Wakili Msomi Andrew Manumbu na Dada Carol Manyama. Tukiangalia kwa undani suala zima la ubakaji ndani ya ndoa na kama kwa sheria zetu za Tanzania swala hili linaweza likajitokeza na endapo likijitokeza nini haswa kinatakiwa kifanyike kuhakikisha vitendo hivi vinakomeshwa mara moja.
Unaweza kupata sheria:
https://rita.go.tz/eng/laws/History%20Laws/Marriage%20Ordinance,%20(cap%2029).pdf
Sheria ya Kanuni za Adhabu
https://tanzlii.org/tz/legislation/act/2019-11
---
Send in a voice message: https://anchor.fm/sheriapoa/message -
Jinsi ya kumiliki eneo ndani ya jengo Tanzania (Unit Titles / Condominium)
Kipindi cha leo ni muendelezo wa mada ya kujua jinsi ya kumiliki ardhi Tanzania. Leo tupo na Wakili Msomi Victor Mwakimi, na mazungumzo ya leo ni kujua hasa jinsi mtu anaweza akamiliki eneo ndani ya jengo. Pia kuzungumzia kuhusu haki azipatazo mtu anayenunua eneo ndani ya jengo au eneo na zile anazopata mtu aliyenunua kiwanja au nyumba na kama kuna utaofauti wowote kati ya wamiliki hawa.
Kujua zaidi kuhusu wawasilishaji;
Victor Mwakimi;
https://tz.linkedin.com/in/victor-mwakimi-5a5188125
https://www.lysonlaw.co.tz/member/vmwakimi@lysonlaw.co.tz
Privaty Rugambwa;
https://www.linkedin.com/in/privaty-patiensi-rugambwa-5078554a/
https://www.irglobal.com/advisor/privaty-patiensi-rugambwa/
Emmanuel Bakilana;
https://tz.linkedin.com/in/emmanuel-g-bakilana-846405123
Kupakua sheria;
The unit titles Act;
http://lands.go.tz/uploads/documents/en/1456495481-The%20Unit%20Titles%20Act%20No.%2016%20of%202008.pdf
---
Send in a voice message: https://anchor.fm/sheriapoa/message -
Mikataba ya wachumba kabla ya Ndoa (Prenups) - Tanzania
Mikataba ya wachumba kabla ya ndoa (Prenups) ni mikataba ambayo wanandoa watarajiwa huingia kuhusu mali walizochuma kabla ya kufungua ndoa husika. Aina hii ya mikataba lengo lake kuu huwa ni kuhakikisha mali ambazo wanandoa wamechuma kabla ya ndoa husika hazitokuwa mali za pamoja za wanandoa hao endapo ndoa hiyo itavunjika.
Katika kipindi cha leo tupo na Wakili msomi Emmanuel Bakilana, ambaye anatufafanulia kuhusu mikataba hii, madhumuni yake, faida na hasara zake kwenye jamii yetu ya kitanzania na sisi kama jamii tunahitaji aina hii ya mikataba.
Kwa maelezo zaidi kuhusu wazungumzaji;
Privaty Rugambwa
https://www.linkedin.com/in/privaty-patiensi-rugambwa-5078554a/
https://www.irglobal.com/advisor/privaty-patiensi-rugambwa/
Emmanuel Bakilana
https://tz.linkedin.com/in/emmanuel-g-bakilana-846405123
Kwa maelezo zaidi juu ya Mikataba ya wanandoa kabla ya ndoa
Kupakua Sheria
The Law of Marriage Act [CAP 29 RE 2019]
https://rita.go.tz/eng/laws/History%20Laws/Marriage%20Ordinance,%20(cap%2029).pdf
Tovuti
https://www.investopedia.com/terms/p/prenuptialagreement.asp
https://www.graysons.co.uk/advice/prenuptial-agreements/
https://brittontime.com/2021/02/22/what-is-a-prenup-and-how-do-they-work/
---
Send in a voice message: https://anchor.fm/sheriapoa/message -
Masuala ya Ardhi katika Mirathi
katika kipindi hiki, tuko pamoja na wakili Victor Mwakimi akiendelea kuzungumzia kwa kina Masuala ya ardhi katika mirathi. Karibu ujumuike nasi.
---
Send in a voice message: https://anchor.fm/sheriapoa/message -
Unyanyasaji wa Kingono kwenye Sehemu za Kazi
Sheria ya kazi na mahusiano ya kazi ya mwaka 2004 kama ilivyofanyiwa maboresho mwaka 2019, imezungumzia kidogo sana juu wa unyanyasi wa kingono kwenye sehemu za kazi. Sheria imeweka unyanyasaji wa kingono chini ya makundi au aina ya ubaguzi mahala pa kazi na hivyo kuonekana kama ni tatizo dogo sana kwenye eneo la kazi na mahusiano ya kazi. Kumekuwa na matatizo mengi sana juu ya tatizo hili la unyanyasaji wa kingono kazini, watu wengi sana wamekuwa wakinyanyaswa na watu mbalimbali ikiwemo waajiri au hata wafanyakazi wenzao na hivyo kusababisha matatizo makubwa sana kwao ikiwemo msongo wa mawazo.
Katika kipindi chetu cha leo kama ilivyo ada, tupo na Dada Chiku Semfuko, ambaye ni Mwanataaluma kwenye maswala ya kinjisia. Chiku amebahatika kufanya kazi sehemu mbalimbali juu ya maswala ya kazi hususan masuala ya unyanyasaji wa kingono kazini. Katika kipindi chetu cha leo tunazungumza nae kinagaubaga juu ya swala hili, ukubwa wa tatizo na nini kifanyike kuweza kupunguza tatizo hili kwenye jamii yetu kwa ujumla.
Kuhusu watoa mada;
Chiku Semfuko
https://tz.linkedin.com/in/chiku-mariam-semfuko-04907b73
Privaty Rugambwa
https://tz.linkedin.com/in/privaty-patiensi-rugambwa-5078554a
Kupakua Sheria ya kazi na Mahusiano Kazini;
https://www.ilo.org/dyn/natlex/docs/ELECTRONIC/68319/104204/F-894240970/TZA68319.pdf
---
Send in a voice message: https://anchor.fm/sheriapoa/message -
Haki za wanyama wafugwao majumbani Tanzania
Sikuhizi imekuwa ni kitu cha kawaida kuona nyumba au watu wakifuga wanyama mbalimbali kama mbwa au paka kama wanyama rafiki, kwa ajili ya majumbani kwa ilinzi au tu kama marafiki. Pia imekuwa ni kama desturi kuona vijana wakiwa wanauza wanyama hawa barabarani au sehemu mbalimbali kwenye miji mbalimbali Tanzania. Kumekuwa na maswali mengi sana kutoka kwa wadau na kwenye mitandao juu ya haki za wanyama wafugwao majumbani na wajibu ya watunza wanyama hawa.
Katika kipindi cha leo, watoa mada wetu leo ni Mawakili Wasomi Ndugu Privaty Rugambwa, na Emmanuel Bakilana wamefanya tafiti juu ya haki za wanyama hawa wafugwao majumbani na katika kipindi cha leo tutapata kujua haki za wanyama hawa na wapi kama jamii tunafanya makosa.
Kujua zaidi kuhusu wawasilishaji;
Deodatus Tesha;
https://tz.linkedin.com/in/deo-tesha-32545776
Privaty Rugambwa;
https://www.linkedin.com/in/privaty-patiensi-rugambwa-5078554a/
https://www.irglobal.com/advisor/privaty-patiensi-rugambwa/
Emmanuel Bakilana;
https://tz.linkedin.com/in/emmanuel-g-bakilana-846405123
Kupakua sheria na nyaraka;
https://www.mifugouvuvi.go.tz/uploads/publications/sw1595835544-Animal%20Welfare%20Act%202008.pdf
https://www.mifugouvuvi.go.tz/uploads/publications/sw1595837886-SERA%20YA%20MIFUGO.pdf
---
Send in a voice message: https://anchor.fm/sheriapoa/message