A life well lived Spiritually, Health, Realatinships and being Rich is a Treasured Possession.

MWALIMU WA NENO UFOO KASSA GEORGE

Be Strong I Every Area of Your Life & Spread Love.

Episodes

  1. SOMOLANNE;- MWANAMKE ANA JUKUMU LA KUURUDISHA UTAWALA WA MUNGU DUNIANI.

    03/20/2021

    SOMOLANNE;- MWANAMKE ANA JUKUMU LA KUURUDISHA UTAWALA WA MUNGU DUNIANI.

    SOMOLANNE:- MWANAMKE ANA JUKUMU LA KUURUDISHA UTAWALA WA MUNGU DUNIANI. MWANZO 3: 14 Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako; 15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino. Msitari wa 15; Mungu ameweka uadui kati ya mwanamke na shetani. Lakini kwa sababu ya roho ya uasi inaitawala dunia bado mwanamke anapenda kulekule kwa shetani kutafuta msaada kwa ajili ya mume wake na watoto na hata familia ya babake na mamake!! Kwa hiyo shetani amekua akitegemewa na wanawake kuleta suluhisho la maisha, wakati huyohuyo shetani ndiye alileta balaa hili zito duniani la kutugombanisha na kututenganisha na Muumba wetu!!?? Hii inawezekana vipi?? Ili mimi na wewe tuweze kuaminiwa na Mungu kurudisha mahusiano ya mwanadamu na Mungu tuliyoyapoteza ni lazima kwanza MWANAKME UTAKASIKE! Uwe na moyo safi. Kama tulivyoanza kwenye somo la kwanza. MATHAYO 5: 8 Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu. Ili uwe na moyo safi huna budi kumpa Mungu nafasi ausafishe na autakase moyo wako. Sababu kama moyo wako si safi 100%, bado shetani anakua ana vitu vyake moyoni mwako, na anaweza kukurudisha tena matopeni na ukatumia vibaya utawala wa dunia uliopewa na Mungu. "Maana watamuona Mungu" Maana yake ni kufunguliwa macho yako ya ndani ufahamu wako kutiwa Nuru kama tunayojifunza hapa. MWANZO 1: 3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. Cha kwanza kama hujaokoka ama hujaamua 100% kumpa Bwana Yesu maisha yako ili alete Nuru kwenye moyo wako. Hili ni jambo la kwanza kabisa Mungu alilifanya katika uumbaji ni kuumba Nuru. Na ili Mungu afanye Kazi zake hapa duniani kupitia mwanamke ni lazima awe ametakasika ndipo Mungu anakua uhakika kuwa hatazuiliwa na hatachafuliwa Kazi yake. Mimi na wewe kama wanawake, wasichana, mke, shangazi, mama mdogo, wifi, shemeji, mama mkwe, nk matendo ama matunda yangu yanaleta Uhai na Uzima popote nilipo?? Wagalatia 5: 22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. MWANZO 3: 6 Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala. Ni vitu vingapi kama mwanamke umemlisha mumeo na ikawa balaa?! Inaweza ikawa; neno, chakula, tendo, nk. Unaweza kuwa kabisa umevitoa kwa wachawi (waganga) au watumishi wa Mungu wa uwongo! MATHAYO 7: 15 Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali. 16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? 17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya. 18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. 19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni. 20 Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua. 1 Yohana 4: 1 Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. SIKILIZA SAUTI 👇🏾👇🏾👇🏾👇🏾👇🏾

    22 min
  2. SOMOLATATU;- CONTACT ME WATSAPP: 0758600428. MIMI KAMA MWANAMKE NI NANI KATIKA UUMBAJI WA MUNGU?

    03/20/2021

    SOMOLATATU;- CONTACT ME WATSAPP: 0758600428. MIMI KAMA MWANAMKE NI NANI KATIKA UUMBAJI WA MUNGU?

    CONTACT ME WATSAPP: 0758600428. MWALIMU WAKO UFOO KASSA GEORGE. MWANZO 2:16 Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, 17 walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika. 18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye. 19 Bwana Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake. 20 Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye. 21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, 22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. 23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume. 24 Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja. 25 Nao walikuwa uchi wote wawili, Adamu na mkewe, wala hawakuona haya. WAFILIPI 2: 5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; 7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; 8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. 9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; 10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; 11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba. YOHANA 16: 7 Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu. 8 Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu. 9 Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi; 10 kwa habari ya haki, kwa sababu mimi naenda zangu kwa Baba, wala hamnioni tena; 11 kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa. 12 Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa. 13 Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake. 14 Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari. 15 Na yote aliyo nayo Baba ni yangu; kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasheni habari.

    34 min

About

Be Strong I Every Area of Your Life & Spread Love.