Neno la Leo

Neno la Leo 255

Hii ndiyo siku aliyoifanya Bwana (Zaburi 118:24). Anza siku mpya ya Yesu kwa kusiliza na kutafakari nasi “Neno la Leo” kila siku kwa lugha ya Kiswahili.

  1. 3d ago

    Usiifiche Karama Ambayo Mungu Ameweka Ndani Yako!

    🎙️ Leo kwenye Neno la Leo Leo kupitia 1 Samweli 10:22 tunakutana na picha ya kushangaza. Wakati umefika wa Sauli kutangazwa mbele ya watu kama mfalme lakini Sauli haonekani. Wanapomtafuta, Mungu anawaonyesha kwamba amejificha miongoni mwa mizigo. Jana tuliona Roho wa Bwana akimjia Sauli na Mungu akimwezesha kwa ajili ya jukumu lililokuwa mbele yake. Leo mtu yule yule ambaye Mungu amemwandaa anajificha. Neno la leo linatufanya tujiulize: Kwa nini wakati mwingine tunakimbia kile ambacho Mungu mwenyewe ameweka ndani yetu? Mungu anaweza kutupa karama, uwezo, nafasi au jukumu lakini hofu, kujiona hatutoshi au kuogopa maoni ya watu kukatufanya tujifiche. Kuna tofauti kati ya unyenyekevu na kujidharau. Wakati mwingine tunasema, “Mimi siwezi, mimi sifai, kuna wengine bora kuliko mimi,” tukidhani ni unyenyekevu wakati kumbe hofu imevaa mavazi ya unyenyekevu. Lakini kuna tahadhari nyingine muhimu katika simulizi ya Sauli. Kupewa uwezo na Mungu hakumaanishi kwamba kila uchaguzi wetu wa baadaye utakuwa sahihi. Sauli atalazimika kuendelea kuchagua utii. Hivyo ujasiri wa kutoka mafichoni lazima uambatane na utegemezi kwa Mungu. Je, kuna kitu ambacho Mungu ameweka ndani yako lakini umekuwa ukikificha kwa sababu ya hofu? Huenda tatizo si kwamba Mungu hajakupa uwezo. Huenda ni kwamba bado hujawa tayari kutoka miongoni mwa “mizigo” yako na kutumia kile alichokupa. Karibu tusikilize, tutafakari na kujifunza pamoja. 🙏📖✨

    Usiifiche Karama Ambayo Mungu Ameweka Ndani Yako!

About

Hii ndiyo siku aliyoifanya Bwana (Zaburi 118:24). Anza siku mpya ya Yesu kwa kusiliza na kutafakari nasi “Neno la Leo” kila siku kwa lugha ya Kiswahili.

You Might Also Like